Saturday, October 8, 2011

MZEE WA SAFARI NAONA ANATAKA KUTOA COLLABO NA SENTI 50


Dah kwa style hii tuna kazi kweli kweli katika hii nchi,huwa nakaa nawaza hii miaka minne iliyobaki itaisha lini maana......nshachoka!

Sunday, August 28, 2011

IT'S MADCHESTER!!!!!!!!!

Wakati manchester city wakiwavurumisha vijana wa london kaskazini kwa mabao 5-1 wallah nilikuwa najiandaa kupata futwari katika mwezi huu mtukufu wa ramadhani karim,baada ya kupata futwari na kuja kuangalia matokeo ya mwisho kati vijana wengine wa mji wa manchester wanaitwa mashetani wekundu dhidi ya Arsenal almanusra futari niitapike it was 8-2.Mara ya mwisho kupata ushindi mkubwa kwa man utd dhidi ya arsenal ni mwaka 2001 kwa bao 6-1.Hii ya sasa ni kaliiiiii!

Wednesday, August 24, 2011

THE FAMILY I ADMIRE!


kumekuwa na tetesi kuwa will smith aka big will style ame split na mkewe jada smith pinket,lakini wanandoa hawa ambao nimiongoni mwa couple wanaotengeneza pesa nyingi kwa mwaka wamekanusha hiyo kitu!

MANCHESTA YUNAITED CLASS OF 2011-2012


Kulikuwa na class of 92 enzi hizo za kina paulo scholesy,David beckham,ryan giggs na wengineo,soccer pundit mmoja anaitwa Alan Hansen akamwambia Ferguson kuwa ''YOu will win nothing with kids'' huo ulikuwa mwaka 95-96.msimu huo manchester wakatwaa taji na mwaka unaofuatia,sasa je hii class of 2011 ya babu fergie itawezaaaa?

Sunday, June 26, 2011

BATA BOYS KAMA KAWA NDANI YA MALAIKA


Ilikuwa usiku wa tarehe 25.06.2011 siku ambayo myamwezi shaggy alikuwa amedondoka mitaa ya mwanza kwa ajili ya kufanya show ya fiesta kwa udhamini mkubwa wa serengeti.so ikawa imeandaliwa party flani hivi kimtindo MEET & GREET. hapa ndo tukawa batani na washkaji.Naonekana kimtindo kushoto kabisa t shirt ya mistari,then wanaoonekana vizuri hapo Rama,g sengo na pembeni yake ni baba jonii,adam mchomvu from clouds fm.

Saturday, June 25, 2011

WILD WILD WEST!


Mwanzoni wakati naitazama hii picha,i was thinking kwamba bado kuna wamarekani wengine wanashanglia kifo cha anko OSAMA hadi leo.Nikashawishika kusoma habari yake ndipo nilipoangalia heading yake nikagundua kuwa inasema hivi.."GAY MARRIAGE APPROVED".Yaani ndoa za watu wa jinsia moja zaruhusiwa huko NEW YORK marekani.Sasa hao kwenye picha ndio wanashangilia baada ya senate kupitisha muswaada huo wa kijinga kuruhusu ndoa za mashoga!